Wednesday, October 31, 2012

Mhando atimuliwa rasmi Tanesco

Habari zilizopatikana juzi usiku na kuthibitishwa na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini na wale wa Tanesco zinasema, Mhando alikabidhiwa rasmi barua ya kuachishwa kazi juzi.

HATIMAYE Serikali imemngíoa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kuanzia juzi jioni.

Uamuzi wa kumwachisha kazi Mhando ulifikiwa katika kikao cha Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika hilo, ambacho kinadaiwa kwamba kilikuwa na mvutano mkali kabla ya kufikia makubaliano.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na bodi hiyo, Mhando ameachishwa kazi baada ya uchunguzi uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kubainisha kwamba alikiuka taratibu za shirika hilo na kujihusisha na matumizi mabaya ya madaraka.

Taarifa hiyo pia ilisema kwamba Mhando ambaye awali, alisimamishwa kazi Julai 16, mwaka huu pamoja na maofisa wengine wa shirika hilo kutokana na tuhuma hizo baada ya kutiwa hatiani, Bodi hiyo ya Tanesco iliunda jopo la watu watatu kusikiliza utetezi wake kabla ya kuchukua hatua ambalo nalo pia lilimtia hatiani.
Bodi hiyo ilikutana Oktoba 29, mwaka huu na kujiridhisha kuwa Mhando alitenda makosa yanayohusiana na kuingia kwenye mikataba yenye mgongano wa kimasilahi kinyume na taratibu za shirika hivyo kufikia uamuzi wa kumwachisha kazi.

Habari zilizopatikana juzi usiku na kuthibitishwa na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini na wale wa Tanesco zinasema, Mhando alikabidhiwa rasmi barua ya kuachishwa kazi juzi.

ìKilichomponza Mhando ni ule mkataba alioingia na mke wake wa Sh800 milioni wa kusambaza vifaa vya ofisini, hilo ndilo lilimponza na kwenye ripoti ya CAG wameweka wazi kwamba kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu za zabuni,î kilisema chanzo kingine.

Mbali na Mhando, bodi hiyo pia iliwasimamisha kazi wafanyakazi wengine watatu ambao ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Robert Shemhilu, Ofisa Mkuu wa Fedha, Lusekelo Kassanga na Meneja Mwandamizi Ununuzi, Harun Mattambo.

Hata hivyo, siku chache baada ya Mhando kusimamishwa kazi liliibuka kundi la watu wakiwamo baadhi ya wabunge, ambao walikuwa wakimtetea kwa madai kwamba alikuwa ameonewa.

Kundi hilo lilikwenda mbali zaidi na kutaka Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Eliakimu Maswi wawajibishwe kwa uonevu huo.

Kadhalika, Profesa Muhongo na Maswi walidaiwa kwamba walimlazimisha Mhando kukiuka Sheria ya Ununuzi wa Umma katika mchakato wa kununua mafuta ya kuendesha mitambo ya umeme wa dharura.

Katika vita hiyo, zilizuka tuhuma kutoka kila upande, mvutano ambao baadaye ulizaa tuhuma kwamba baadhi ya wabunge walihongwa ili kukwamisha bajeti ya wizara hiyo.†

Tuhuma hizo zilisababisha Spika wa Bunge, Anne Makinda kuivunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, kisha kuunda kamati ndogo ya kuchunguza tuhuma hizo za rushwa dhidi ya wabunge.

No comments:

Post a Comment