Wednesday, October 31, 2012

‘Ijumaa iwe siku ya mapumziko’

“Mbunge wa chama cha upinzani anatoa mchango wake anaambiwa kaa chini hata kama ana mchango mzuri kiasi gani… Spika akiwa kwenye chama fulani inaleta mpasuko”alisema.
Pia alitaka Katiba Mpya iweke kifungu kitakachoilazimisha Tume ya Uchaguzi (NEC),

MKAZI wa Kijiji cha Kikwe wilayani Siha, Halima Munisi ametaka katiba ijayo iitambue siku ya Ijumaa kuwa ni siku ya mapumziko kama zilivyo siku za Jumamosi na Jumapili.
Munisi alitoa pendekezo hilo juzi wakati akitoa maoni yake mbele ya kamati ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa ikiongozwa na Profesa Mwesiga Baregu.
Kwa mujibu wa mwananchi huyo, Ijumaa kutokuwa ni siku ya mapumziko hasa kwa kuwa ndio siku ya kumuabudu Mola kwa Waislam si sahihi na kutaka siku hiyo iwe ya mapumziko.
Mkazi wa Kitongoji cha Nasai, Stanslaus Mallya alitaka katiba ijayo iweke kifungu ili Mawaziri watakaoteuliwa katika Baraza la Mawaziri wasiwe wabunge wa kuchaguliwa wala kuteuliwa.
Mallya alisema kitendo cha Mawaziri kushika kofia mbili ya Uwaziri na Ubunge, kinawafanya wasitekeleze majukumu yao ipasavyo hasa pale inapofikia mahali pa kuibana Serikali.
Kwa upande wake mkazi wa Ndoroso, Solomon Mmari alitaka Spika wa Bunge asiwe Mbunge na wala kuwa mfuasi wa chama chochote cha siasa ili aweze kutenda wajibu wake kwa haki.
Hoja hiyo iliungwa mkono na Radegunda Nyabu, mkazi wa Magadini Bomang’ombe ambaye alisema endapo Spika anatokana na chama cha siasa, kuna kila sababu ya kutoa upendeleo.
“Mbunge wa chama cha upinzani anatoa mchango wake anaambiwa kaa chini hata kama ana mchango mzuri kiasi gani… Spika akiwa kwenye chama fulani inaleta mpasuko”alisema.
Pia alitaka Katiba Mpya iweke kifungu kitakachoilazimisha Tume ya Uchaguzi (NEC), kutopanga siku ya uchaguzi kwa siku zile ambazo zinatumika kumwabudu Mungu.
Kwa mujibu wa Nyabu, siku hizo ni Ijumaa kwa waumini wa Kiislam na Jumamosi na Jumapili kwa waumini wa Kikristo ili kila mmoja aweze kumwabudu na kumtukuza mola wake.

No comments:

Post a Comment